Mwanamuziki kutoka Nigeria amewataka mashabiki zake kuacha kumuita mtoto wake wa kike ‘Duduke’.
Wakati alipokuwa kwenye mahojiano na ‘VJ Adams’ Simi amewasihi mashabiki zake kuacha kumuita mtoto wake jina hilo kwani linamkera na halina maana yoyote.
“Watu wengine humwita binti yangu Duduke jambo ambalo sipendi. Hilo si jina lake na halina maana yoyote, sipendi.
Kama ingekuwa na maana nzuri kama ‘baraka’, hiyo ingekuwa sawa. Lakini Duduke ni sauti tu du du ke sauti ya ngoma, hiyo ndiyo nilimaanisha. Nilimaanisha moyo wangu unapiga kama ngoma. Tafadhali acheni kumwita mtoto wangu Duduke,”amesema Simi
Kwa takribani miaka 5 mashabiki wamekuwa wakimuitwa mtoto huyo Duduke baada ya msanii huyo kutoa wimbo ambao Simi aliimba kwa ajili ya kutangaza ujauzito wake wakati wa janga la Corona ambapo mpaka kufikia sasa wimbo huo umetazamwa zaidi ya mara milioni 80 kupitia Youtube.
Mtoto huyo ambaye jina lake kamili ni Adejare ‘Deja’ Simi alimpata mtoto huyo na mume wake mwanamuziki Adekunle Gold.

Leave a Reply