Mwigizaji Michael B. Jordan ameeleza kuwa moja ya jambo ambalo analikumbuka siku zote ni ushauri alioupokea kutoka kwa Denzel Washington ambapo alimsihi kuepuka mitandao ya kijamii.
Wakati alipokuwa kwenye mahojiano na Vulture mwigizaji huyo wa Sinners ambaye aliwahi pia kuigiza katika filamu ya ‘A Journal for Jordan’ mwaka 2021 iliyoongozwa na Washington ambapo alimtaka kuacha kujiposti sana katika mitandao ya kijamii hasa katika zama hizi.
“Kwanini walipie kukuona katika filamu zako kila wikiend kwenye sinema, wakati wanakuona wiki nzima bure. Acha kushiriki vitu vyako mitandaoni,”amesema Jordan
Aidha mwigizaji huyo ameeleza kuwa jambo hilo limemfanya kujikita katika kazi zake na kuachana na mitandao ya kijamii pamoja na kiki.
Kwa sasa Jordan anatamba na filamu ya Sinners iliyoongozwa na Ryan Coogler ambayo imeendelea kufanya vizuri huku ikikusanya jumla ya dola 352.2 milioni duniani kote.

Leave a Reply