Mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini ambaye pia ni mkali wa Singeli, D Voice amewataja wasanii ambao anatamani kuwasaini endapo ataanzisha lebo ya Singeli.
Wakati alipokuwa kwenye mahojiano na moja ya chombo cha habari Mkoani Shinyanga alipokwenda kwa ajili ya ziara yake ‘D Voice Tour’ ameeleza kuwa atawasaini wasanii kama Meja, Sajent na wengineo.
“Endapo nitafungua lebo ya Singeli nitamsaini, Kiwanda, Sele Minamba, Dakota mtu hatari, Stizo naye ni mtu hatari, Monta D, Dony blee ni mkali anatokea Mbagala, Sajenti nitamchukua kama Chino atanikubalia, Dulla Makabila, Meja na Dogo Elisha.
Kwahiyo hapo nikiwa na hiyo timu inakuwa singeli nzima naimiliki mimi wengine nawaachia wao, mtu yoyote akitaka kushindana na mimi inabidi ajipange,”amesema D Voice
Utakumbuka kabla ya kusaiiniwa katika lebo ya Wasafi mwaka 2023 D Voice alitambulika kupitia muziki wa singeli akitoa ngoma kama Madanga ya mke wangu, Danga usitume meseji, Masela, Umekopwa na nyinginezo.

Leave a Reply