Ishu Ya D Voice Na Meja Kunta Ilikuwa Hivi

Ishu Ya D Voice Na Meja Kunta Ilikuwa Hivi

Msanii wa Singeli nchini D Voice, ameweka wazi tuhuma alizopewa na msanii mwenzake Meja Kunta kuhusu kumuibia wimbo 'Ex wa Nani' na kumpatia Jux

D Voice amesema wimbo huo ni wake na ameuandika tangu 2019 lakini uongozi wa Meja Kunta ulikataa wimbo huo kutoka wakidai ni mbaya.

D Voice ameyasema hayo leo Juni 4, 2025, alipokutana na waandishi wa habari wakati akitambulisha ziara yake ya muziki 'D Voice Tour 2025' inayotarajiwa kuanza Juni 6, 2025.

"Ngoja niliweke sawa hili swala kwa sababu sikutaka kulizungumza kwa muda mrefu. Ningependa nitoe ushauri kwa kaka zangu na wasanii wote wa Singeli. Mimi nafanya muziki ni biashara kwa sababu ndio inaendesha maisha yangu. Sina biashara nyingine nje ya muziki inapokuja kwenye sekta ya kazi yangu nahitaji umakini kidogo uwepo.

"Kuhusiana na Meja Kunta nilifanyanae wimbo unaitwa 'Ex wa Nani' nimeurekodi wimbo huo toka mwaka 2019. Mimi na nyimbo nimezirekodi tangu 2018 na ninazo kichwani, niliamua kurekodi ule wimbo nikamtafuta mara ya kwanza nikamwambia nina wimbo wangu tukaenda studio tukarekodi.

Nikamtumia meneja wake ‘Waso Wiso’ akasema wimbo hajaupenda nikawauliza mnauhakika huu wimbo ni mbaya wakanambia kutokana na vipaji vyenu mnaweza kufanya wimbo mkubwa zaidi ya huu, nikauchukua ule wimbo mbaya uliokataliwa nakaamua kuuimba na Jux," amesema D Voice.

Amesema hakumpa taarifa Meja Kunta wakati wimbo huo unatoka kwa sababu wimbo ni wake na yeye ndio anachagua wa kufanya naye.

"Nilimpigia Meja akalalamika kwanini sikumpa taarifa. Nikamwambia sijakupa taarifa kwasababu wimbo ulikataliwa na Menejimenti yako na tayari tumefanya wimbo mwingine upo. Kwahiyo niliona hakuna haja ya mimi kutoa taarifa kwa sababu wimbo haupo kwenye mahesabau yenu na wimbo ni wangu nina haki ya kuuimba kokote na msanii yeyote ninaye mtaka," amesema D Voice.

Aidha D Voice amezungumzia sakata la ndoa ya Diamond na Zuchu akisema hata yeye alishtuka kuona taarifa ile kama wengine.

"Ndio Wasafi tupo kama familia lakini mimi siwezi kuacha kuhakikisha Tour yangu inaendaje, kwa sababu dakika za mwisho kinachotukutanisha sisi ni kazi na hakuna tajiri anayempenda mfanyakazi wake asiyempa faida yoyote. Mimi nilikuwa napambania ndoto zangu sikupata muda mrefu wa kukaa na Simba na kujua kama ameoa kwahiyo nilishtuka pia kama nyie mlivyoshtuka," amesema D Voice.

Amesema muziki wa Singeli kwa sasa upo sehemu nzuri unahitaji watu wenye nguvu ili kuushika mkono ufike mbali zaidi.

"Singeli inajitosheleza lakini kitu tunahitaji ni kupata watu wenye nguvu zaidi ili watusaidie kupushi zaidi. Mfano kama Jux, leo hii Nigeria watu wanaimba na kucheza na hatukuimba Kingereza lakini kwa sababu ni mtu mwenye ushawishi, ndiyo maana leo hii nina Singeli mbili na Zuchu, nimefanya na Diamond, nimefanya na Jux tupo kwenye mkakati ili watu waone na wakishatutengezea nafasi sisi tunashambulia tuu," amesema D Voice.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags