Davido Asusia Shoo London, Ataja Sababu

Davido Asusia Shoo London, Ataja Sababu

Mkali wa Afrobeat kutoka Nigeria, Davido ameelezea sababu za kujiondoa kwenye shoo iliyopangwa kufanyika Tottenham Hotspur Stadium jijini London Julai 3, 2025, akisema sababu ni kutokuwepo kwa ubora, na usalama katika eneo hilo.

“Kwa wiki kadhaa nimejitahidi kutoa ushirikiano wa hali ya juu kwa ‘The Necto Future Group’, lakini bado kuna changamoto katika utekelezaji wa vipengele muhimu vinavyohusiana na ubora na usalama wa shoo yangu," ameandika Davido.

Davido ameongezea kuwa shoo hiyo itafanyika lakini hatokuepo, pia amesema uamuzi huo ni mgumu lakini amelazimika kuufanya kwa heshima ya sanaa yake, mashabiki wake, na utamaduni anaouwakilisha.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa ziara ya albamu yake mpya ya ‘5ive’ bado inaendelea kama ilivyopangwa katika nchi mbalimbali zikiwemo Ujerumani, Ureno, Ubelgiji, Kanada na Marekani.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags