Adaiwa kufariki baada ya mwalimu kumlazimisha afanye mazoezi

Adaiwa kufariki baada ya mwalimu kumlazimisha afanye mazoezi

Mwanafunzi wa miaka 12, Yahshua Robinson anadaiwa kufariki dunia baada ya mwalimu wa mazoezi kumlazimisha mtoto huyo kufanya mazoezi ya kukimbia katika kipindi cha joto kali.

 

Mtoto huyo ambaye alikuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Canyon Lake, California, alianguka asubuhi wakati akikimbia kama mwalimu wake alivyomtaka afanye mazoezi.

 

Ndipo alianguka chini uwanjani na kuhitaji msaada wa maji, wakati akiendelea kupatiwa huduma ya kwanza alizidiwa na kuzimia, kisha kukimbizwa hospitalini ambako ndiko alipoteza maisha, ikidaiwa kuwa chanzo ni mshituko wa moyo.

 

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post