WMO yatahadharisha ongozeko la joto katika nchi mbalimbali

WMO yatahadharisha ongozeko la joto katika nchi mbalimbali

Shirika la utabiri wa hali ya hewa la Umoja wa Mataifa,WMO limesema joto litaongezeka kwa kiwango kikubwa kutokana na mchanganyiko wa athari za joto la baharini na hewa zinazochafua mazingira katika nchi mbalimbali.

Kwa mujibu wa shirika hilo, dunia inapaswa kujitayarisha kwa sababu kuna uwezekano wa asilimia 98  wa joto kuwa kali mno.

Nae katibu Mkuu wa shirika hilo la utabiri wa hali ya hewa la Umoja wa Mataifa, Petteri Taalas, amesema mfumo wa joto wa El Nino unatarajiwa kujijenga katika miezi ijayo na hali hiyo itachanganyika na athari za mabadiliko ya tabia nchi zinazosababishwa na binadamu na kuielekeza dunia katika mkondo usiotabirika.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post