Wanaume 11 waliombaka mjamzito kuachiwa huru India

Wanaume 11 waliombaka mjamzito kuachiwa huru India

Hii bwana imetokea huko nchini India ambapo Wafungwa 11 waliokuwa wamehukumiwa Kifungo cha Maisha kwa Ubakaji na mauaji nchini humo kumezusha maandamano huku Mwathiriwa wa Ubakaji akitoa wito kwa Serikali kubatilisha uamuzi wake, akisema uamuzi huo umetikisa Imani yake katika Haki.

Aidha Bilkis Bano alikuwa na ujauzito wa miezi mitano wakati wa ghasia zilipotokea mwaka 2002 katika Jimbo la Gujarat, ambapo alibakwa na Kundi la Wanaume 11.

Hata hivyo Wanaume hao wameachiwa huru Agosti 15, 2022 baada ya Serikali ya Jimbo kuidhinisha ombi lao la kuondolewa adhabu huku kuachiliwa kwao kukiambatana na Sherehe za Uhuru wa Nchi hiyo.

Unaweza kutoa maoni yako hapo chini kuhusiana na sakata hili la huko nchini India funguka.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post