Viatu vitakavyo ongeza muonekano katika mavazi yako

Viatu vitakavyo ongeza muonekano katika mavazi yako

It’s furaidayyy!! I hope uko poa mwanangu sana kama kawaida sisi nia na dhumuni letu kukupasha yale yote unayoyasikia na unayo yajua kwa uchache katika uwanja wa fashion tuna kujuza zaidi.

Leo katika kapu letu la fashion nimependa nikusogezee kitu ambacho this weekend utajifunza kitu mwanetu, hivi unajua fashion ina bebwa na muonekano, Team Scoop ina mengi sasa ngojea tuzungumzie kwanza viatu vitakavyoongeza muonekano katika mavazi yako.

Ni nani anayeweza kumlaumu mwanamke kwa kuweka kabati lake la nguo kutoka juu hadi chini na viatu, kwanza kabisa kuna mitindo na rangi zisizo chuja au kupitwa na wakati katika viatu, mwongozo huu utakufundisha jinsi ya kuchagua viatu vya kuvaa na vazi bila kujali rangi ya mavazi, tukio au msimu.

  • Chagua rangi za viatu zinazofanana na nguo zako

Hapa unaweza kuvaa viatu vyovyote unavyopenda na vinavyoendana na nguo yako mradi hakuna kanuni ya mavazi ya kutii au masuala ya afya na usalama ya kuzingatia.

Zingatia visigino au gorofa zisizoegemea upande wowote au aina ya nguo ya jioni inayometameta. Mfano ukivaa kiatua cheusi ni rahisi kwa kuvalia mtindo wowote wa mavazi au rangi yoyote.   

  • Kwa mavazi ya kawaida vaa viatu vinavyo ng’aa

Ongeza aina ya viatu vya rangi kwa kulinganisha mavazi yako yalio na rangi za kupoa itakuletea muonekano mzuri, hapa sasa, utajaribu kiatu chenye muundo mzuri mfano kiatu cha ngozi, ikiwa umevaa blauzi nyepeze au ya mterezo na suruali na suluali fupi ya jeans.

 

  • Epuka kumechisha rangi

Usivae rangi moja kwanzia juu hadi chini, ikiwa una blauzi ya blue na skirt ya blue, epuka kuvaa viatu vya rangi hiyo hautapata muonekano wenye kupendeza.

Hapa watu wengi huwa wanafeli kwa kumechi full kama askali kanzu wa enzi za mkoloni kwa mantiki hiyo huwezi kuwa wa kuvutia machoni kwa watu na uta onekana waajabu.  

  • Chagua rangi za kawaida

Hapa usitake makuu sana kwasababu katika mitindo kuna hitaji mpangilio hivyo chagua rangi za kawaida za viatu ambazo zitakufanya uwe na muonekano nazifu.

Hakuna kitu kizuri kama kujihisi hali ya kujiami pale unapopangilia mavazi yako hadi kiatu, hapo kama unaenda kwenye sherehe unakuwa na muanekano wakipeke na kama unavyojua mwanamke akipendeza kwanzia juu hadi chini huwa anajijua bhana. 

  • Chagua viatu sahihi kwa msimu

Unaweza kuchagua viatu vya msimu wa baridi na viatu vya kiangazi kadiri nguo zako zinavyobadilika hadi majira ya kuchipua.

Kama majira ya joto ni wakati wa kufurahia viatu vyako vya espadrilles (viatu vya nguo) viatu vya aina hiyo ukivaa vinapitisha hewa na vinafanya miguu yako kuto dhoofika kwaajili ya joto.

Kwa majira ya baridi chagua loafers (kiatu cha ngozi), hakikisha kwamba hiko kiatu kisigino chake kiwe kipana ili kuepusha kuteleza wakati wa mvua.

Bado unaweza kunyumbulika hata kwa majira ya baridi, lakini epuka viatu na espadrilles kwasababu hazifanani na vitambaa vizito na rangi ya vuli.

  • Oanisha viatu vya stiletto (viatu vyenye visigino virefu)

Nguo ambazo tayari husaidia kurefusha mguu wako, kama vile sketi za penseli na suruali nyembamba Stiletto hujenga udanganyifu wa urefu zaidi, na kufanya miguu yako iwe myembamba zaidi na yenye kuvutia.

Hasa kwa watu wenye vyimo vifupi viatu vya kisigino virefu inapendeza kwa nguo ndefu ina msaidiahiyo nguo kuonekana vizuri.

Tumia viatu vya kisigino ili kufanya nguo za kawaida zionekane nzuri zaidi kwa mfano, jaribu kuunganisha pea ya viatu vya kisigino na sketi ya kawaida ya cotton na blauzi ili kufanya vazi liwe laini zaidi.

Mara nyingi viatu vinavyo valiwa na sketi ndefu zinaweza kumfanya mwanamke aonekane mchafu kama hato zingatia aina ya kiatu ambacho anatakiwa avae kutokana na mtindo wa sketi yake.

Ikiwa unavaa viatu vya visigino na sketi ndefu utakuwa na muonekana bora.



  • Vaa viatu vya riadha vilivyoundwa kwa ajili ya mchezo

Ikiwa wewe ni mkimbiaji, mwana michezo au unafanya mazoezi unatakiwa hapa uvae viatu husika vya michezo, kwa mfano, vaa viatu vya kukimbia vya insoles (kiatu cha mazoezi).

Huwezi ukavaa buti za kawaida kwajili ya michezo kwasababu kuna viatu ambavyo haviwezi kuhimili mikiki kama insoles hivi vinakuwa special kwajili ya kukusadia kufanya mazoezi ukiwa cormfortable.

Kwa mantiki hiyo itoshe kusema kwamba fashion ni maisha ya kila siku mwanetu sisi kama Team Mwananchi Scoop tunalithibitisha hilo na ndio maana tunakujuza kipya kila weekend basi isiwe tabu kukuambia tukutane next weekend kwaajili ya mambo mapya katika fashion.   

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post