Moja ya kitu ambacho kilikuwa kinasubiriwa kwa hamu kwenye muziki wa Tanzania ni kumuona msanii mkongwe, anayependwa, na mwenye ushawishi mkubwa kwenye tasnia hiyo, Ali Salehe Kiba 'Alikiba' akifanya muziki wa Singeli ambao ndio nembo ya nchi hii inayotambulika Kimataifa kwasasa.
Alikiba ambaye anaheshimika kama 'Mfalme wa Bongo Fleva,' yupo mbioni kuachia wimbo wake wa kwanza wa Singeli, aina ya muziki ambayo inawakilisha mitaa ya jiji la Dar es Salaam, na kusambaa sehemu mbalimbali za dunia.
Hivi karibuni, Kiba ameachia kionjo cha wimbo huo utakaofahamika kama 'Ubuyu,' ujio wake huo hauashirii tu mageuzi yake binafsi kama msanii, bali unaashiria wakati muhimu kwa muziki wa Singeli na mafanikio makubwa kwa muziki wa Tanzania.
Hatua hii ya kimkakati ya mmoja wa wasanii mashuhuri zaidi wa Afrika Mashariki inaweza kuunda upya mipaka ya muziki, na kuinua sauti za wasanii wachanga wa muziki huo katika hatua kubwa zaidi.
Umuhimu wa jina “Ubuyu” na maana yake ya kitamaduni
Jina la "Ubuyu" lina mguso na maana kubwa Kitamaduni hapa Tanzania ambayo inatokana na lugha ya Kiswahili, neno hilo likimaanisha uvumi au porojo tamu, kwa lugha nyepesi wenyeji huita 'umbea', Kwa kuchagua jina hili, Alikiba anagusa kipengele kinachohusiana na maisha ya kijamii ya kila siku ya Mtanzania.
Chaguo la jina hilo katika wimbo huo linaonesha asili ya Singeli kama aina ya muziki iliyozaliwa kutoka mitaani. Kukubalika kwa Alikiba kwa neno hilo aliloupatia wimbo wake inaashiria nia yake ya kujihusisha kiuhalisia na mizizi ya kitamaduni ya Singeli badala ya kuhusika kwa sauti yake pekee.
Ujio wa wimbo wa 'Ubuyu' unawakilisha ujio wa aina yake kwa Alikiba, ambaye amezoeleka katika uimbaji wake kupitia nyimbo za Bongo Flava na R&B.
Hatahivyo, huu ndio wimbo wa kwanza wa Singeli kwa Alikiba, lakini yeye sio msanii wa kwanza wa Bongo Fleva kuja na wimbo wa singeli, wapo waliotangulia kufanya hivyo ambao ni Zuchu, Diamond Platnumz, Harmonize, Mbosso, Rayvanny, Jux na wengine wengi.

Leave a Reply