Spider Man wa bongo Amkera Wema Sepetu

Spider Man wa bongo Amkera Wema Sepetu

Moja ya story ni hii ya aliyewahi kuwa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu ameweka wazi kukerwa na Spider Man wa Bongo ambaye anatrend mitandaoni akicheza taarab na kuuza matunda barabarani.

Wema ambaye pia ni msanii wa filamu ameshea hisia zake kwa Spider Man wa Bongo baada ya comment yake kwenye page ya Esma Platnumz aliyom-post Spider Man akimpa ushauri kuhusu nguo yake ya ndani.

Wema aka-comment kwenye page hiyo kwa kuandika 'Simpendi' jambo ambalo limefanya mashabiki wengi kumshambulia Wema kwa kutoa comment hiyo.

Tuambie na wewe msomaji wetu jambo gani linakukera kwa Spider Man wa bongo, tupia comment yako katika ukurasa wetu wa Instagram ambao ni @mwananchiscoop.






Comments 1


  • Awesome Image
    Jonas

    hana ubaya.. mbona yupo poa tu.. anafurahisha na kuwapa hamasa vijana wengi kujaribu kufanya chochote halali kupata kipato au umaarufu utakaoweza kumpa kipato..Hao wakina wema walikuwa maarufu marakadhaa kwa kufanya mambo ya hovyo hadharani.. madawa ya kulevya n.k aaache kuwa na ubongo mdogo

Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post