Sho Madjozi atoa funzo kwa wanamuziki wa Tanzania

Sho Madjozi atoa funzo kwa wanamuziki wa Tanzania

Mwanamuziki #ShomaDjozi amefunguka kuwa wasanii wa Afrika Kusini wana sample nyimbo zao za zamani ili kutoa muziki mzuri wakisasa Amapiano, lakini kwa wasanii wa Tanzania hawafanyi hivyo.

Aidha Katika kuthibitisha  kauli yake  alionesha kwa vitendo akitumbuiza jukwaani  akiimba wimbo wake mpya wa Amapiano ambao amechukua sample kutoka kwa mkongwe wa muziki Tanzania Matonya kupitia wimbo wake ‘Anita’.

Shomadjozi ameonekana mara kadhaa kuupigania muziki wa Bongo Fleva akifanya kolabo na baadhi ya wasanii wa kitanzania na  kuonekana kufanya vizuri kwenye hizo nyimbo alizoshirikishwa na wasanii kutoka Tanzania.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post