Shindano la kumpata mtu muongo zaidi duniani

Shindano la kumpata mtu muongo zaidi duniani

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni, wakati baadhi ya watu wakikemea vikali tabia ya kusema uongo, fahamu kuwa kila mwaka ifikapo Novemba, katika mji wa Santon, Uingereza, hufanyika shindano la kumtafuta mtu muongo zaidi duniani "The World's Biggest Liar.".

Katika shindano hilo washiriki wanapima uwezo wao wa kusema uwongo kwa njia ya ubunifu na kufurahisha. Licha ya kuwa shindano hufanyika Uingereza lakini washiriki hutoka sehemu mbalimbali dunia.

Shindano hilo limewekwa kwa lengo la kuburudisha na kukuza vipaji vya watu katika kusema hadithi za uwongo. Kawaida wakati wa shindano hilo washiriki hutunga hadithi za uongo na kuzisimulia mbele ya jopo la waamuzi.

Kanuni na sheria za shindano washiriki wanapaswa kuwasilisha hadithi zao za uongo kwa wakati, na kila mmoja anapewa dakika chache kuhadithia uongo jukwaani. Uongo huo unaweza kuwa wa hadithi yoyote lakini inapaswa kuwa ya kujenga na kuhamasisha.

Washindi hupatiwa tuzo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na medali na heshima katika jamii. Pia, washindi wanapewa nafasi ya kuandika hadithi zao kuziwasilisha katika majukwaa majukwaa ya burudani






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post