Sexyy Red: nitakuwa nimekosema kumpa Drake jukumu la malezi

Sexyy Red: nitakuwa nimekosema kumpa Drake jukumu la malezi

Baada ya ‘rapa’ Sexyy Red na mwanamuziki Drake kuonesha ukaribu kwa siku za hivi karibuni mwanadada huyo amewauliza swali mashabiki wake kama ni sawa kumpa jukumu la malezi ya mtoto wake Drake.

#SexyyRed kupitia ukurasa wake wa X alianza kwa kumshukuru Drake kwa kumshirikisha kwenye albumu yake ‘For All The Dogs’ huku akiuliza mashabiki wake kuwa ni sawa yeye kumpa Drake jukumu la malezi ya mtoto wake, hii inakuja baada ya wawili hao kuwa na ukaribu wa kupitiliza katika kipindi cha ujauzito.

Ikumbukwe kuwa hata hivyo #Drake hausiki na ujauzito wa #SexyyRed, kwani mwanadada huyo alishawahi kum-post Baby Dady wake lakini hakuweza kumuonesha sura yake.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post