Scott kuzindua albamu Piramidi, Misri

Scott kuzindua albamu Piramidi, Misri

Rapa kutoka nchini Marekani Travis Scott ametangaza kuzindua albamu yake mpya alioipa jina la ‘Utopia’ kwenye show atakayoifanya Piramidi za Giza nchini Misri Ijumaa hii.

Utopia itakuwa albamu ya kwanza ya Travis Scott baada ya tamasha la muziki la Astroworld 2021 huko Houston, linalokumbukwa kwa kuacha majonzi baada ya vifo vya watu kadhaa na kujeruhi wengine.

Aidha Bad Bunny anatajwa kuwa ni miongoni mwa wasanii walioshirikishwa kwenye albamu hiyo, baada ya kuonekana na Briefcase yenye jina la albamu na Mnigeria Rema ambao walionekana wakishoot video huko Kano, Nigeria wiki kadhaa nyuma.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post