Sadio ajenga uwanja nyumbani kwao

Sadio ajenga uwanja nyumbani kwao

Nyota wa ‘timu’ ya Taifa ya #Senegal, na ‘klabu’ ya #AlNassr #SadioMane, amejenga uwanja wa mpira wa miguu katika kijiji alichozaliwa cha Casamance, Kusini mwa nchi ya Senegal.

Inaelezwa kuwa jana Jumatano Mane amezindua uwanja huo, uliyopewa jina la ‘Stade de Bambali’, uliojengwa kwa kiwango cha kimataifa katika sehemu ya kuchezea (pitch).

Hii si mara ya kwanza kwa Sadio kukumbuka mahali alipozaliwa mwaka 2021alijenga hospitali iliyopewa jina la ‘L hospital De Bambaly’ na kutoa misaada mbalimbali kwenye shule.

.

.

#MwananchiScoop

#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post