Ramos bora angekubali kadi ya njano

Ramos bora angekubali kadi ya njano

Katika mchezo kati ya ‘klabu’ #Sevilla dhidi ya #RealSociedad inadaiwa kuwa mchezaji wa ‘klabu ya Sevilla, #SergioRamos alimuomba muamuzi akaangalie kwenye VAR uwezekano wa kufuta kadi ya pili ya njano lakini akajikuta anaambulia kadi nyekundu.

Inaelezwa kuwa muamuzi alikubali alipoenda kuangalia akaona faulo aliyofanya mchezaji huyo aliporudi akaifuta kadi ya njano akampa nyekundu ya moja kwa moja.

Mechi hiyo ilichezwa siku ya Jumanne ilimalizika kwa bao 2-1 ambapo ‘timu’ ya Real Sociedad iliibuka na ushindi.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post