Priyanka aelezea livyopata changamoto katika upasuaji ( surgery)

Priyanka aelezea livyopata changamoto katika upasuaji ( surgery)

Ebanaeee!! haya mambo ya upasuaji kwadhumuni la kubadilisha muonekano itawatoa watu roho sasa, bhana muigizaji wa filamu kutoka bollywood nchini India Priyanka Chopra amefunguka jinsi alivyokumbwa na msongo wa mawazo katika upasuaji. Baada ya Daktari aliyemfanyia upasuaji wa kurekebisha pua kukosea

Priyanka amezungumza na moja ya chombo cha habari nchini India na kuweka wazi kuwa

"Ulikuwa ni wakati mmbaya sana kwangu maana uso wangu ulikuwa tofauti nikapata msongo wa mawazo nilipunguzwa kushiriki kwenye filamu tatu tofauti jambo ambalo niliona ndio mwisho wa kipaji changu cha uigizaji" alisema Priyanka

Hata hivyo Priyanka amesema kuwa Marehemu Baba yake Ashok Chopra hakuwa nyuma alimtia moyo na kuwa nae bega kwa bega mpaka aliporudia kufanya upasuaji mwengine ambao hapo alipata kile alicho kuwa nahitaji.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post