Peter wa P-square apandikizwa nywele Uturuki

Peter wa P-square apandikizwa nywele Uturuki

Mwanamuziki kutoka Nigeria Peter Okoye a.k.a Mr P ameweka wazi kuwa amefanyiwa upasuaji wa kupandikizwa nywele uliyofanyika jijini Istanbul, nchini Uturuki.

Kufuatia na video inayosambaa mitandaoni inaeleza kuwa ameamua kufanya upasuaji huo kutokana na kutopendezwa na muonekano aliyokuwa anao huku akidai kuwa nywele zake zilianza kutoka na kuwa kipara.

Hata hivyo kupitia ukurasa wake wa Instagram alithibitisha kuwa takriban nyuzi 2,400 za nywele zilitolewa kutoka sehemu tofauti ya kichwa chake na kupandikizwa kwenye maeneo yenye upara.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post