Cappuccino ni kinywaji cha kahawa chenye vipimo sawa vya espresso, maziwa ya moto, na maziwa yaliyopigwa (milk foam). Kinywaji hicho kimejizolea umaarufu katika nchi nyingi ikiwemo Tanzania na kuwafanya baadhi ya watumiaji wake kutoboa mifuko yao zaidi ya wanywaji wa kahawa ya kawaida ili kukipata.
Jambo la kufurahisha ni kwamba unaweza kuandaa kinywaji hiki nyumbani hata kama hauna vifaa au mashine ambazo mara nyingi hutumika katika migahawa kuandaa kinywaji hicho. Mbali na kutengeneza nyumba kwa ajili ya familia lakini pia inaweza ikawa furasa kwako na kuibadilisha kuwa biashara ambayo itakuingizia maokoto.
MAHIAJI
- Sukari au vanilla (hiari)
- Maziwa ya fresh robo kikombe
- Maziwa yaliyochemshwa kiasi
- Chupa ya plastiki kwa ajili ya kupigia au kutikisa maziwa
- Kahawa vijiko viwili
NAMNA YA KUTENGENEZA
Chukua kikombe weka vijiko viwili vya kahawa ya unga na maji kidogo (kama 1/4 kikombe) ili kutengeneza kahawa nzito kama espresso. Kisha ishemshe kikasi mpaka utakapoina ni nzito kabisa. Au unaweza kuchukua kahawa, sukari na maji ya moto kiasi ukakoroga mpaka pale kahawa yako itakapokuwa nzito. Weka pembeni.
Kahawa yako ikiwa tayari chukua nusu kikombe cha maziwa weka kwenye sufuria pamoja na sukari kiasi kisha yapasha moto lakini yasichemke (yawe ya uvuguvugu tu, si zaidi ya 70°C).
Utayaweka pembeni kisha utachukua maziwa mengine kiasi utayatia kwenye chupa ya plastiki na utaaza kuyapiga au kuyatingisha kwa nguvu mpaka yawe na mapovu.
Baada ya hapo utachanganya vitu vyako vyote vitatu kwa mtiririko huu. Ambapo utaanza na kumimina kahawa kwenye kikombe, kisha Mimina maziwa ya moto juu ya kahawa kwa taratibu na baadaye utamalizia kumimina maziwa yako yenye povu (milk foam).
Endapo utataka kutengeneza maua basi wakati unapomimina maziwa yako yenye povu basi utatakiwa kuyaweka taratibu huku ukiwa unatengeza urembo unaouhitaji kama ambavyo baadhi ya video zinaonesha katika mitandao ya kijamii.
Na mpaka kufikia hapo kahawa yako ya maziwa au cappuccino itakuwa tayari unaweza kunywa na vitafunwa kama cake, bite nk. Lakini pia inaweza ikawa fursa kwako msaomaji wetu kwa kuifanya kuwa biashara itakayokuingizia pesa.
Leave a Reply