Mtihani wa mwisho waziponza shule 34  India

Mtihani wa mwisho waziponza shule 34 India

Kutoka huko nchini India bwana ambapo Mamlaka za Jimbo la Assam zimefikia uamuzi wa kufunga Shule 34 na kuhamishia Wanafunzi wa katika shule nyingine baada ya kufanya vibaya katika mitihani.

Hii imekuja baada ya Wanafunzi wote kufeli mtihani wa mwisho ambapo Maelfu ya Wanafunzi kutoka Shule mbalimbali za Jimbo hilo walifanya Mitihani ya Cheti cha Kumaliza Elimu ya Sekondari ambapo zaidi ya Wanafunzi 1,000 kutoka Shule 34 zilizofungwa walifeli mtihani huo.

Hata hivyo Wazazi, Walimu pamoa na Wadau wa Elimu wamekosoa uamuzi huo na kusema  kuwa hauna mantiki.

Aiseeee unaweza kudondosha comment yako hapo chini kuhusiana na sakata hilo lilitokea huko nchini India.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post