Monalisa aomba radhi

Monalisa aomba radhi

Kimeumana huko mwigizaji wa filamu yvone cherrie maarufu kama monalisa amewaomba radhi watanzania na mashabiki zake kwa ujumla baada ya mtoto wake Sonia kutoa kauli ilioleta gumzo kwenye mitandao ya kijamii hususani Instagram.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram monalisa ameachia ujumbe mzito akiwaombaa radhi watanzania juu ya kauli aliyo izungumzaa binti yake wakati akifanyiwa mahijiano na chombo cha habari. Na kueleza kuwa

‘’ Kama mzazi, nimeumizwa na mapokeo ya watu baada tu ya kukitazama kipande kifupi na sio interview nzima. Lakini kikubwa kilichoniumiza ni Wasafi kukazia kwenye Caption yao kwamba "Hakuna chuo chochote anachokifahamu Bongo"lakini wameacha kabisa kwamba amevitaja Vyuo anavyovifahamu kikiwemo UDSM na IFM ambavyo yeye alikuwa anavitazamia kusoma maana anasoma masomo ya BIASHARA’’  alisema

‘’1.Sonia ni mtoto wa mama ambaye ni maarufu. Mambo mengi sana yanamzunguka kwenye hili, wewe unayecomment matusi sidhani kama umeliwaza hili.’’

‘’2.kubali au kataa, hili jambo lipo sana tu nikiwa kama mzazi niliyekulia jiji hili najua, WABABA mnatuharibia mabinti zetu wa Chuo .Hata kama mtoto amelelewa vipi, vishawishi hivi vyaweza kuwa vigumu kuviepuka.’’ Aandika Monalisa






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post