Mavazi na mitindo ya 'fashion' hubadilika haraka, na kile kilichokuwa maarufu jana, leo kinaweza kuonekana cha kupitwa na wakati au hata kuchefua watu. Mitazamo kuhusu fashion inayoonekana inachukiza au imepitwa na wakati hutegemea sana muktadha wa kijamii, umri, na mazingira.
Zifuatazo ni baadhi ya mitindo ambayo watu wengi kwa sasa huiona kama haivutii au imepitwa na wakati.
Jeans zenye matobo mengi kupita kiasi
Kwa lugha ya kimitindo huitwa Ripped jeans au crazy jeans, ambapo huwa na matobo makubwa hadi miguu yote inaonekana, huonekana kuchukiza na kupitwa na wakati.
Mavazi yenye Logo kubwa, Haya ni mavazi yenye majina ya kampuni au Brand za mavazi ambazo zimeandikwa kwa ukubwa kama GUCCI au LV kwenye kifua kizima. Watu wengi wanaona aina hiyo inalenga kuonyesha hadhi, na sio fashion.
Jeans za kubana (Skinny jeans) kwa wanaume,
Aina hiyo ya mavazi kwa wanaume suruali zikiwa zimebana sana miguu huchukiza na sio ya kupendeza na ni mitindo iliyopitwa na wakati kwasasa watu wengi wanapendelea bwanga au Suruali za kuachia mwili
Nguo zenye rangi nyingi (Matching Set)
Kwa mfano, kuvaa top, suruali, viatu na kofia vyote rangi ya green au pink, au Yellow inakuwa haipendezi na huchukiza zaidi watu wanaweza kukuona mshamba, kwa sababu ni mitindo iliyopitwa na wakati
Mavazi yenye maneno ya kejeli au lugha chafu za matusi
T-shirts au hoodies ( Sweta) zilizoandikwa maneno ya kukera, kejeli au matusi kwa lengo la kuhitaji kupata attention ni mambo yaliyopitwa nawakati.
Kuvaa nguo nyingi za Brands tofauti tofauti kwa wakati mmoja
Mfano unakuta mtu kavaa makampuni mengi kama GUCCI, Prada, Louis Vuitton vyote kwa wakati mmoja inahesabiwa kama 'overbranding' napia hupoteza thamani na uzuri wa mavazi hayo.
Leave a Reply