Mhamiaji awa meya Marekani

Mhamiaji awa meya Marekani

Mhamiaji kutoka nchini Nigeria Yemi Mobolade ameapishwa Juni 6 kuwa meya wa kwanza mwenye asili ya kiafrika nchini Marekani katika jiji la pili kwa ukubwa la Colorado.

Gavana wa jimbo hilo la Colorado Jered Polis alisema ametiwa moyo na wasifu wa kuvutia wa Mobolade.

“Mtu ambaye amejitolea maisha yake na kuifanya Colorado Springs na Amerika kuwa mahali pazuri zaidi, mwenye historia ambayo wote tunaweza kuielewa, amekuja hapa, na kuanzisha biashara.” Alisema Polis wakati wa sherehe ya kuapishwa kwake.

Aidha baadhi ya wakazi walisema kuwa ushindi wa Mobolade katika uchaguzi unatuma ujumbe kwamba jimbo lao linakaribisha watu kutoka matabaka yote ya maisha.

Mobolade alihamia nchini Marekani miaka 27 iliyopita akiwa mwanafunzi na akawa raia wa nchi hiyo mwaka wa 2017.

Alianzisha familia, akafungua migahawa miwili na kanisa, kisha akashinda uchaguzi katika jiji hilo akiwa kiongozi wa kwanza mweusi kuchaguliwa katika jiji hilo.anasema.

“Ninapoamka kila asubuhi ninadhani nipo ndotoni, halafu nagundua, hapana, jambo hili ilitokea kweli” Mobolade alisema.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post