Mfahamu binadamu mwenye ngozi inayovutika zaidi

Mfahamu binadamu mwenye ngozi inayovutika zaidi

Gary Turner ambaye ni raia wa Uingereza anashikilia rekodi ya dunia ya Guinness kuwa binadamu mwenye ngozi inayovutika zaidi duniani.

Turner mwenye umri wa miaka 56 aliweka rekodi hiyo baada ya kufanikiwa kuivuta ngozi yake kwa inchi 6.25 mwaka 1999, nchini Marekani katika mji wa Los Angles.

Kupitia uwezo wake huu alifanikiwa kuigiza kwenye movie iitwayo ‘He Took His Skin Off For Me’ na amekuwa akijiingizia kipato kupitia matamasha mbalimbali ya kuonesha uwezo wake huo.

Turner aliwahi kuwa kwenye ndoa na mwanamke aliyefahamika kwa jina la Carli Norris mwaka 2005 na walipeana talaka mwaka 2014.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post