Mbinu anayotumia Chris Brown kukumbuka mistari stejini

Mbinu anayotumia Chris Brown kukumbuka mistari stejini

Mwanamuziki kutoka Marekani Chris Brown ameweka wazi kuwa anaposahau mistari ya nyimbo zake akiwa stejini huwa anawaachia mashabiki waimbe.

Brown ameyasema hayo kwenye moja ya mahojiano yake baada ya kuulizwa swali kama amewahi kusahau baadhi ya mistari ya ngoma zake akiwa stejini, na ndipo akaeeleza kuwa tatizo hilo huwa linamtokea mara kwa mara hasa akiwa kwenye zaira zake.

“Kila mara ninaposahau nyimbo zangu jukwaani huwa nageuza kipaza sauti (mic) kwa mashabiki na kuwaacha waimbe”

Hata hivyo kwa mujibu wa msanii huyo amedai kuwa huwa anasahau mistari ya nyimbo hizo kutokana kwa sababu ya kuwa na ngoma nyingi ambazo amezitoa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post