Mawigi, Kope bandia kuongezewa kodi, Kenya

Mawigi, Kope bandia kuongezewa kodi, Kenya

Hahahahahhaha! Make hapa kwanza ncheke, hivi majirani zetu wanaweza kuvumilia hili maana sio powa, basi bwana unaambiwa mawigi, kope bandia vyapandishwa kodi.

Hazina ya kitaifa nchini Kenya kupitia muswada wa Fedha ambao utawasilishwa Bungeni hivi karibuni imependekeza makampuni ya betting kulipa kodi za bidhaa (ED) kwa mamlaka ya mapato nchini humo (KRA) ndani ya masaa 24 huku mawigi, nywele na ndevu za bandia pamoja na nyusi na kope vikitakiwa kutozwa ushuru wa asilimia 5 ya mauzo.

Aidha simu zinazotoka nje ya nchi pia zitatakiwa kutozwa ushuru wa asilimia 10. Haya watu wangu wa nguvu dondosha komenti yako hapo chini kwa bongo ni kitu gani cha bandia kiongeze kodi?.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post