Mastaa ambao tayari wamewasili nchini humo ni pamoja na msanii wa Bongo Fleva Ommy Dimpoz, Jimmy Chansa, Poshy Queen, Mc Garab, pamoja na familia ya msanii Juma Jux.
Harusi hiyo ya kitamaduni ni moja kati ya mfululizo wa zile sherehe za baada ya ndoa yao iliyofanyika Februari 7, 2025. ambapo alitangaza kuzifanya mwaka huu nchini Nigeria na Tanzania.

Baada ya harusi hiyo ya kitamaduni Jux na mkewe wanatarajia kufanya tafrija nyingine Mei mwaka huu nchini ambapo itahusisha ndugu, jamaa, Marafiki, mashabiki na watu wengine wa karibu.
Hata hivyo, Jux na mke wake wamekuwa Nigeria tangu Machi, ambapo walihudhuria uzinduzi wa filamu ya Labake Olododo ambayo imechezwa na mama mzazi wa priscilla, Iyoboojofespris.
Leave a Reply