Marioo: Mwaka wa tatu nawakimbiza kwa ngoma kali

Marioo: Mwaka wa tatu nawakimbiza kwa ngoma kali

Mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini, Marioo amejipa maua yake kwa kudai kuwa yeye ndiyo msanii anayekimbiza zaidi katika bongofleva kwa kuwa na ngoma kali.

Marioo ameyaeleza hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameandika kuwa

“Huu Mwaka wa Tatu Mfululizo Nawakimbiza kwa Kuwa Na Nyimbo Nyingi Kali na Hits, Kwenye Hizo Chats zenu Mnazoziaminia “i know you know that i’m the best, Na hata kwenye Tuzo Ikitokea Michezo kama ya Msimu Uliopita, Nitaendelea Kupeleka Moto”

Kwa sasa msanii huyo anatamba na kibao chake cha ‘Hakuna Matata’ pamoja na ngoma aliyoshirikishwa na Harmonize iitwayo ‘Disconnect’ ambayo inakimbiza katika mitandao ya kuskiliza muziki.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post