Lava Lava atoa shukrani kwa wasanii nje ya wasafi

Lava Lava atoa shukrani kwa wasanii nje ya wasafi

Mwanamuziki wa bongo fleva nchini Lava Lava ametoa shukrani kwa baadhi ya wasanii ambao wamemtafuta na kumpongeza baada ya kuachia ngoma zake mbili.

Lava Lava kupitia ukurasa wake wa Instagram ame-share ujumbe wa kutoa shukrani ambapo ameeleza kuwa ni mara ya kwanza kwa wasanii wenzake nje ya Wasafi kusifia project ya ngoma zake mbili alizoziachia.

Siku ya jana Februari 9 Lava Lava aliachia nyimbo mbili ambazo ni ‘Sawa’ na ‘Pambe’ mpaka kufikia sasa wimbo wa ‘Sawa’ unazaidi ya watazamaji elfu tisa huku wimbo wa ‘Pambe’ ukiwa na wasikilizaji elfu 24 kwenye mtandao wa #Youtube.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post