Konda amuua abiria aliyepungukiwa nauli

Konda amuua abiria aliyepungukiwa nauli

Ukisoma kichwa cha habari unaweza ukashtuka lakini ndio ukweli kwamba konda amekatisha uhai wa abiria wake aliyepungukiwa nauli huko nchini Kenya.

Tukio hilo limetokea Jumatano Mei 17 katika Barabara ya Outering iliyoko jijini Nairobi, ambapo mzozo uliibuka kati ya konda na abiria huyo mwenye umri wa miaka 17 aliyepungukiwa kiasi cha nauli cha KSh 20.

Inadaiwa mabishano yalizidi kati ya konda na abiria huyo hivyo konda akaamua kumtupa nje wakati gari hilo likiwa kwenye mwendo, kwa bahati mbaya gari hilohilo ndilo lililomkanyaga na kumuuwa.

Inadauwa konda aliyetekeleza tukio hilo alikimbia ndipo wanachi wenye hasira kuamua kulichoma moto gari hilo






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post