Kocha wa Bayern aitamani saini ya Gomez

Kocha wa Bayern aitamani saini ya Gomez

Kocha wa klabu ya #BayernMunich, #VincentKompany anaisaka saini ya beki wa klabu ya #Liverpool, #JoeGomez ili awe mmoja wa wachezaji wake wa kwanza kusajiliwa katika kikosi chake msimu ujao.

Kwa mujibu wa gazeti la The Mirror, limeeleza kuwa ubora wa Gomez uwanjani umemvutia Kompany wakati huu ambao anajiwekea mikakati ya kuimarisha safu ya ulinzi ya Bayern.

Hata hivyo ‘kocha’ aliyeondoka #Liverpool, #JurgenKlopp alikuwa akimchezesha mchezaji huyo katika nafasi za beki wa kati, kushoto, nyuma, kulia na hata katikati na hii inaweza kuwa sababu kubwa kwa mwalimu Vincent Kompany kutamani huduma yake.

Gomez mwenye umri wa miaka 27 raia wa Ungereza alisajiliwa Liverpool Julai 1 nwaka 2015 ambapo mkataba wake unatarajia kumalizika June 30 mwaka 2027.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post