Kocha mkongwe awakosoa makocha wa kizazi kipya

Kocha mkongwe awakosoa makocha wa kizazi kipya

‘Kocha’ mkongwe wa ‘klabu’ ya #RealMadrid, #CarloAncelotti amedai kuwa ‘makocha’ wa kizazi kipya wanafanya makosa kwa wachezaji wao kwenye utoaji wa maelekezo.

Carlo huyo ambaye ni mshindi mara nne wa ‘ligi’ ya mabingwa Ulaya amebainisha kuwa kumpa mchezaji maelekezo mengi pindi awapo na mpira uwanjani ni kumuondolea ubunifu.

Hata hivyo ameeleza kuwa kumpa mchezaji maelekezo kuhusu nafasi awapo uwanjani akiwa hana mpira ni jambo zuri maana hapo lazima utoe maelekezo ya kutosha kwa sababu akiwa hana mpira kinachozingatiwa ni umakini, kujitolea na kucheza kwa umoja.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post