Kinyesi cha Twiga chamuweka matatani mwanamke mmoja

Kinyesi cha Twiga chamuweka matatani mwanamke mmoja

Mwanamke mmoja amekamatwa kwenye Uwanja Wa Ndege Wa Minnesota nchini Marekani, akiwa na kinyesi cha Twiga kutoka nchini Kenya.

Mwanamke huyo alieleza kuwa alibeba kinyesi hicho kwa lengo la kutengeneza mikufu kama ukumbusho wa safari yake ya Kenya.

Hata hivyo kutokana na tukio hilo Mkurugenzi wa Ustawi wa Forodha na Ulinzi wa Mipaka wa Chicago, LaFonda D. Sutton-Burke, alidai kuwa kuna  hatari kubwa za kiafya zingetokea kama  mwanamke huyo angetengeneza bidhaa hizo kwa kutumia kinyesi cha mnyama huyo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post