Kimeumana,‘Kocha’ wa Azam Fc akumbana na TFF

Kimeumana,‘Kocha’ wa Azam Fc akumbana na TFF

Inadaiwa kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemzuia rasmi ‘Kocha’ mkuu wa ‘klabu’ ya Azam FC, Youssouph Dabo, raia wa Senegal kusimama kwenye 'benchi' la ufundi la ‘timu’ hiyo kutokana na sababu za kutokidhi vigezo ambavyo vinatakiwa.

Dabo ambaye tangu ametua nchini amekuwa akikiongoza kikosi hicho amezuiwa kutokana na "leseni" A ya UEFA aliyonayo kutokidhi vigezo vya kanuni za 'soka' la Tanzania ambazo haziruhusu kuwa ‘kocha’ mkuu wa ‘Ligi’ kuu katika ‘timu’ hiyo.

Inadaiwa TFF imetoa tamko kuwa Dabo hatambuliki kama ‘kocha’ mkuu hivyo kutokana na ‘leseni’ aliyonayo anaruhusiwa kusimama 'benchi' akiwa msaidizi na viongozi wa #Azam tayari wanalijua hilo.

 

Source: Sports Arena
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post