Kesi mauaji ya AKA yaanza kusikilizwa

Kesi mauaji ya AKA yaanza kusikilizwa

Ikiwa imepita siku moja tangu jeshi la polisi nchini Afrika Kusini kutangaza mbele ya waandishi wa habari kuwa limewakamata watu sita wanaotuhumiwa kwa mauaji ya rapa, Kiernan Forbes maarufu AKA, hatimaye watano kati yao leo Februari 29 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Jijini Durban.

Kati ya watuhumiwa wa kesi hiyo yumo anayedaiwa kuwa alihusika kutafuta silaha na usafiri, muandaaji wa tukio, watumia bunduki wawili na wawili waliokuwa wakitoa taarifa.

Majina ya watuhumiwa hao ni Siyanda Myeza (21), Lindokuhle Ndimande (29), Lindani Ndimande (35), ambao ni mtu na kaka yake, Lindokuhle Thabani (30) na Mziwethemba Myeza (36).



Ikumbukwe AKA (35), aliuawa kwa kupigwa risasi Februari 10, mwaka jana, alipokuwa akitembea na rafiki yake nje ya mgahawa maarufu wa Durban, Afrika Kusini.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post