Joe ajutia kumnyima ‘Kolabo’ Drake

Joe ajutia kumnyima ‘Kolabo’ Drake

Msanii kutoka Marekani #FatJoe amuomba msamaha, #Drake kwa kuwahi kumnyima collable ya kufanya nae remix ya wimbo wa ‘All The Way Up’ wimbo ambao aliufanya mwaka 2017.

Ilikuwa baada ya Drake kusikia ngoma hiyo alimpigia simu Joe na kumuomba amtumie mdundo huo ili aingize mistari yake kwa ajili ya Remix.

Rapa huyo wakati akiomba msamaha ameeleza kuwa Drake alikuwa na shauku kubwa ya kutaka kufanya ngoma hiyo, kwani akukuwa akimpigia simu hadi usiku wa manane lakini hakutaka kumsikiliza, hadi pale Drake alipoamua kufanya remix na #Jay-Z.

Fat Joe anadai kuwa Drake alionyeshwa kuchukizwa na kitendo hicho kwani hakuwai tena kumtafuta kwa ajili ya kazi.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post