Mtoto wa Rais wa awamu ya tano, hayati John Magufuli, Jesca Magufuli amesema enzi za uhai wa baba yake alipenda kusikiliza nyimbo za mwanamuziki Timbulo.
Jesca wakati akifanya mahojiano na Millard Ayo amesema baba yake hakuwa mpenzi sana wa mpira wa miguu lakini alipendelea kusikiliza muziki mara kwa mara.
“Mpira alikuwa anaangalia lakini sio shabiki kindakindaki kwamba anaamka anaenda kuangalia mpira hapana. Muziki alikuwa akisikiliza sana alikuwa anachanganya anasikiliza ya zamani na kisasa nakumbuka mzee wangu alikuwa anampenda Timbulo nyimbo zake alikuwa anazisikiliza sana,” amesema Jesca Magufuli
Timbulo amejizolea umaarufu kwa nyimbo zake mbalimbali kama vile Domo Langu, Tamu, Unanionaje, Niende Zangu na nyinginezo.
Utakumbuka, hayati Magufuli alifariki dunia Machi 17, 2021 akiwa na umri wa miaka 61.Kifo chake kilitangazwa na Makamu wa Rais wa wakati huo, Samia Suluhu Hassan, ambaye alichukua nafasi ya Urais kwa mujibu wa katiba.

Leave a Reply