J.Cole ajuta kumuongelea vibaya Kedrick

J.Cole ajuta kumuongelea vibaya Kedrick

Mwanamuziki kutoka nchini Marekani J.Cole amemuomba msamaha Kendrick Lamara katika onesho la Dream Ville usiku wa kuamkia leo.

Cole ameeleza kuwa anajuta kumuongelea vibaya ‘rapa’ huyo kwenye wimbo wake mpya wa ‘7Minute Drill’ ambao upo katika albumu yake mpya iitwayo ‘Might Delete Later’ iliyotoka Jumamosi, April 6.

Kupitia wimbo huo mpya Cole alimchana Kendrick kuwa amepotea kwenye game ila baada ya kutoa wimbo wake wa ‘Diss’ ndiyo mashabiki wameanza kumfuatilia.

Ikumbukwe pia wawili hao wamewahi kufanya nyimbo za pamoja kama ‘Black Frida, ‘Like That’, ‘temptation’, ‘The Millennials Folklore’ na ‘Forbidden Fruit’.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post