Fanya hivi kama simu yako imeingia  kwenye maji

Fanya hivi kama simu yako imeingia kwenye maji

Niaje mtu wangu wa faida leo ni jumatano ya Smartphone nataka kuchonga na wewe jambo hapa unaweza ukawa mwangalifu sana ila, bahati mbaya inatokea na simu zetu zinaingia maji.

Ebwana  eeeh!! Unaweza ukavurugwa kwa dakika kadhaa ukifikiria usawa tulionao na kupata simu nyingine sio poa!, Sasa, kwa kuwa simu zisizoingia maji bado ni ghali sana, simu yako ikiingia maji unaweza ukaiokoa kwa kufanya yafuatayo.

  1. kwanza itoe kwenye maji
  2. Kisha izime halafu ilaze kwenye kitambaa laini au tishu nzito halafu toa kava la nyuma na betri (kama unaweza kufungua simu yako)
  3. Pia, ondoa SIM card, memory card, kava za simu uziache zikauke.
  4. Kausha simu kwa ndani kwa kutumia kitambaa laini au tishu nzito, Hakikisha unaikausha haraka iwezekanavyo.
  5. Weka simu ya ndani ya mfuko wa mchele kwa masaa 24. Mchele unanyonya maji.
  6. Angalia kama eneo la kuchomeka chaji na headphone zimekauka. Kama bado, rudia hatua 4 na 5.
  7. Baada ya masaa 24, jaribu kuiwasha alafu angalia kama ina fanya kazi inavyotakiwa.

Kuna uwezekano kwamba utabidi kuipeleka kwa fundi

Ukiona kwamba haifanya kazi baada ya kupitia hatua hizi, bora uipeleke kwa fundi.

 Ipeleke kwa wakala wa aina ya simu (au mtandao) wa simu yako au kwa duka la kutengeneza vifaa vya umeme linaloaminika.

Ila, kuzuia ni bora zaidi ya tiba, Kwa hiyo, nunua kava ya simu inayozuia maji kuingia kwenye simu.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post