Drake Amtukana Mwanasiasa Kisa Kendrick

Drake Amtukana Mwanasiasa Kisa Kendrick

Rapa kutoka Canada, Drake amerushiana maneno na mmoja wa wanasiasa nchini humo, Jagmeet Singh baada ya mwanasiasa huyo kuhudhuria tamasha la Kendrick Lamar na SZA lililofanyika jijini Toronto.

Kiongozi huyo wa zamani wa 'New Democratic Party' alipigwa picha kwenye tamasha la Kendrick, likiwa ni tamasha lake la kwanza katika mji alikozaliwa Drake.

Baada ya Drake kuona picha alizama kwenye DM ya Singh Instagram, na kumtolea matusi kisha mwanasiasa huyo aliweka ujumbe huo kwenye InstaStory yake.

Aidha mwanasiasa huyo alionekana kuomba msamaha kwa Drake akisema kuwa alienda kwenye tamasha hilo kwa sababu ya SZA na sio Kendrick, na pia anaamini Drake yupo juu kuliko Kendrick.

“Nilienda kwa ajili ya SZA, sio Kendrick. Nilizaliwa katika jiji hili Toronto. Nalipenda jiji hili. Lakini kiukweli, naelewa, sikupaswa kwenda kabisa. OVO na Drake wameinua jiji hili, itakuwa daima Drake atakuwa juu ya Kendrick,”aliandika Mwanasiasa huyo.

Drake bado anaonekana kutomsamehe mwanasiasa huyo kwani amemuanifolo kwenye mitandao yake ya kijamii.

Utakumbuka hivi karibuni Kendrick alitumbuiza matamasha mawili huko Toronto akiwa na SZA ambapo Alhamisi, Juni 12, 2025 Kendrick hakucheka na wowote wala kufanya mabadiliko yoyote kwenye mpangilio wa shoo yake.

K.Dot alitumbuiza wimbo maarufu wa "Not Like Us" na ulipokelewa kwa kishindo kwenye ardhi ya Canada, Drake alipozaliwa huku mashabiki wakiimba kwa sauti wimbo huo mwanzo hadi mwisho.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags