Diamond kununua Ndege yake binafsi

Diamond kununua Ndege yake binafsi

Mambo yanazidi kuwa mazuri kwa upande wa msanii wa muziki nchini Nasibu Abdul maarufu kama Diamond baada ya kutangaza kununua ndege yake binafsi mwaka huu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram akimtakia heri ya siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa meneja wake Sallam Sk, Diamond amesema kuwa atanunua ndege mpya binafsi mwaka huu 2022.

Ujumbe huo ulionekana kupokelewa kwa furaha na mashabiki zake ambao wamemtia moyo na kumwambia kila jambo linawezekana chini ya jua na hakuna kushindwa wa kufeli ukitia nia na kuweka malengo.

Eee bwana hii kubwa sana kutoka kwa msanii wetu tuambie msomaji wetu na wewe una maoni gani katika hili.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post