Diamond ataka wimbo wa enjoy aliyofanya na Jux ufutwe

Diamond ataka wimbo wa enjoy aliyofanya na Jux ufutwe

Mwanamuziki Juma Jux kupitia ukurasa wake wa #Instagram ametoa shukurani kwa mashabiki waliyo pokea wimbo wa #Enjoy aliyofanya na #DaimondPlatnumz kwa kuandika,

“Shukhurani zetu za dhati ziwafikie mashabiki wetu wote wanaoupigania mziki wetu mzuri mnatutia nguvu sana! Asanteni na tunawapenda”

Baada ya shukurani hizo zilizotolewa na #Jux, nyota wa muziki Tanzania #diamondplatnumz hakukaa kimya na kuifikia post hiyo kwa kugongelea misumari akidai kuwa wafute wimbo huo maana wakitoa video itakuwa trending hadi mwaka 2030.  Kwenye comment Diamond aliandika,

“Kwa Support na Upendo Huu mkubwa tunaoupata, mimi naona labda tutumie uungwana tui-delete tu nyimbo …maana nikiwaza na video inakuja basi naona Trend itakua hadi Mwaka 2030”






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post