Diamond akabidhiwa muongozo wa maadili

Diamond akabidhiwa muongozo wa maadili

Baada ya msanii Diamond Platnumz kushinda Tuzo ya MTV EMA 2023 alitembelea katika ofisi za Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) na kukabidhiwa muongozo wa maadili katika kazi za Sanaa kutoka kwa Katibu Mtendaji BASATA, Dkt Kedmon Mapana siku jana Novemba 6.

Kupitia ukurasa wa Instagram #BASATA wame-share picha zikionesha msanii huyo akikabidhiwa muongozo huo huku #Diamond akitoa shukurani kwa viongozo hao kwa kumkabidhi mwongozo na kuahidi kufuata muongozo huo wa maadili katika kazi zake za Sanaa.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post