Davido awapa onyo wanaosambaza picha zake za zamani

Davido awapa onyo wanaosambaza picha zake za zamani

Mwanamuziki kutoka nchini #Nigeria, Davido kupitia mtandao wake X amewapa onyo wanaosambaza picha zake za zamani mtandaoni zikimuonesha akiwa na mkewe hospitali.

Picha hizo zimekuwa zikiambatanishwa na taarifa zinazodai kuwa amepata watoto mapacha hivi karibuni.

Hata hivyo msanii huyo bado hajathibitisha au kukanusha uvumi huo wa kupata watoto mapacha na mkewe Chioma lakini ametoa onyo hilo kwa watu kuacha kutumia picha hizo za zamani.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post