Dababy atoa freestyle ngoma ya Wizkid

Dababy atoa freestyle ngoma ya Wizkid

Unaambiwa huko mitandaoni moja ya story inayogonga vichwa ni freestlye aliyoitoa msanii wa Marekani Dababy kupitia ngoma ya msanii Wizkid inayoitwa Essence.

Dababy amedondoka na freestyle hiyo hii leo baada ya kuonekana akibanjuka siku za hivi karibuni akiimba na ku-share video katika ukurasa wake wa Instagram.

Ngoma hiyo ya Essence imeonekana kuwavutia mastaa wengi nchini Marekani kutokana na ladha lakini pia kilichofanywa na star huyo na kumfanya kuingia katika orodha ya mastaa waliopagawa na mkwaju huu.

Hata hivyo ngoma hii ya Essence ambaye ni ya nne katika album ya ‘Made in Lagos’ imeweka rekodi ya kuwa ngoma ya kwanza toka nchini Nigeria kuingia kwenye chart za Billboard Hot 100.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post