Chuchu Hansy: Nipo njia panda kuolewa na Ray

Chuchu Hansy: Nipo njia panda kuolewa na Ray

Mwigizaji wa filamu nchini, Chuchu Hansy anaonesha kubaki njia panda kila linapokuja suala la kuolewa na mwigizaji  Ray Kigosi.

Akizungumza na Mwananchiscoop, Chuchu amesema anashindwa kuelewa Ray amemuweka kwenye nafasi ipi licha ya kudumu naye kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka kumi.

"Mimi mwenyewe sielewi Ray ameniweka kwenye nafasi gani kama atanioa au maana ameshanitumia karibu miaka 15 kwa hiyo imefikia mahala nakuwa sijiamini,"amesema 

Mwigizaji huyo ameongezea kuwa akimuangalia Ray anaona nia yake ya kutaka kumuoa lakini bado hajataka kuthubutu kufanya maamuzi hayo. 

"Anaonesha nia ya kuoa lakini kuthubutu ndiyo shughuli" amesema Chuchu. 

Amesema licha ya kuwa na matamanio ya kupata ndoa kama wanawake wengine,  hajawahi kufikia hatua ya kutumia ushirikina ili aoelewe na Ray kama watu wanavyosema.

 

"Kama hiyo ipo basi mimi ningekuwa nimeshaolewa kwa sababu ni miaka mingi nimekuwa naye. Kwahiyo naamini mwenyezi Mungu akipenda na kama nimeandikiwa haijalishi napitia nini tutazunguka ila tutarudi na kuwa pamoja,"amesema Chuchu. 

Hata hivyo ameelezea kuhusu baadhi ya machapisho yake ya hivi karibu kupitia ukurasa wake wa Instagram  yanayoonesha akipitia magumu kwenye mahusiano yake na Ray.

"Niseme tu mahusiano yana mambo mengi sana huwezi kuwa na furaha kila siku. Hamuwezi kucheka kila siku, lakini pia kuna muda inafika kama binadamu inakuwa ni kinyongo unatoa niliamka nikajikuta najisikia hivyo ila mwenzangu aliamka vizuri na akaandika sio kila mwanamke ni wakuoa," amesema Chuchu.

 Amesema kwa sasa haamini tena mwanaume atayejitokeza na kutaka kumuoa kwani anaweza kuwa amemtamani baada ya kuona anakaribia kusimamisha mjengo wake mpya. 

"Kiukweli siamini mwanaume kwa sasa sababu baada ya kuachia taarifa ya nyumba yangu siwezi jua mtu anakuja kwa mapenzi au, natamani tubaki kwanza na baba watoto tuchezeshane," amesema.

Amesema nyumba hiyo anayoijenga Kibada, Kigamboni inazaidi ya miaka miwili na alifikia maamuzi ya kujenga mwenyewe baada ya kuona Ray hataki kumuelewa.

Nikiwa kama mwanafamilia, kwasababu mimi na yeye tumeunga damu  lazima nijisikie vibaya watu wanavyosema baba watoto wangu anaishi kwa wazazi wake lakini pia sio kitu kibaya kwa sababu yule hajaoa " amesema Chuchu.

 

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags