Cardi B afunguliwa mashtaka

Cardi B afunguliwa mashtaka

Aliyepigwa na Cardi B afungua mashtaka kwa kitendo cha rapper huyo kumrushia microphone wakati wa onyesho la msanii huyo.

Tukio hilo limetokea weekend iliyopita ambapo mmoja kati ya mashabiki alimmwagia kinywaji Cardi B, wakati akitumbwiza jukwaani, na ndipo rapper huyo alirusha microphone kwa lengo na kumpiga shabiki huyo ambaye alikuwa mwanamke.

Inaelezwa kuwa microphone hiyo haikufika moja kwa moja kwa mlengwa bali ilifika pia kwa mwanamke mwingine, hivyo basi hadi sasa bado haijafahamika kati ya wawili hao waliofikiwa na microphone hiyo ni yupi hasa amefungua shitaka hilo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post