Burba boy: sina tatizo na Davido

Burba boy: sina tatizo na Davido

Eee bwana! unaambiwa moja ya story huko mitandaoni inayobamba ni hii hapa ya msanii wa Burnaboy kuweka wazi kuwa wamemaliza tofauti kati yake na msanii Davido.

Unaambiwa kuwa kwa sasa wawili hao wapo sawa kabisa na hakuna tena bifu kama ilivyokuwa hapo zamani.

Taarifa za kumalizika kwa tofauti hizo zimethibitishwa na Burna Boy ambapo ameshare taarifa hiyo katika Insta Story yake kwa kuandika “Sina tatizo na Davido, tuko sawa, 2022 tunatakiwa tupendane kwa lazima, mbele daima nyuma mwiko,”

Najua wewe ambaye ni mshabiki wa wasanii hawa wawili utakuwa umefurahi sana, basi tudondoshee comment yako katika ukurasa wetu wa Instagram ambao ni @mwananchiscoop.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post