Utafiti: Love Bite Inaweza Kusababisha Kiharusi

Utafiti: Love Bite Inaweza Kusababisha Kiharusi

Kwa mujibu wa utafiti uliyofanywa na madaktari Dkt. Richard Wright, Dkt. Lee Schwamm, Umebaini kuwa ‘Love Bite’ (alama ya busu shingoni) inaweza kusababisha ugonjwa wa Kiharusi.

Utafiti huo unaeleza kuwa love bite kwenye shingo inaweza kusababisha kuganda kwa damu ambayo husafiri hadi kwenye ubongo na kupelekea kupata kiharusi.

Hata hivyo kumekuwa na kesi mbalimbali kuhusiana na tatizo hilo ambapo. Mwaka 2016 kijana kutoka Mexico mwenye umri wa miaka 17 aitwaye Julio Macias Gonzalez, alifariki baada ya kupata kiharusi kutokana na Love Bite aliyoipata kwa mpenzi wake.

Lakini pia mwaka 2010 New Zealand Mwanamke mwenye umri wa miaka 44 alipata ugonjwa wa kupooza kwa kupata love bite shingoni ambapo aliwahiwa hospitali na kupona.

Kesi nyingine iliripotiwa katika jarida la matibabu la PubMed, ambapo mwanamke mwenye umri wa miaka 35 alipata kiharusi saa 12 baada ya kupata love bite huku uchunguzi ukionesha kuwa love bite ilisababisha kuganda kwa damu na kusababisha kiharusi.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags